Kikundi
cha WANAMATU (Wanawake Na Maendeleo Tunaweza) kimeazishwa rasmi Tarehe 8/5/ 2013,
ni kikundi ambacho
kinalengo la kumuinua mwanamke na maendeleo yake(mfano: sherehe, misiba,
ugonjwa na biashara).
MADHUMUNI
A.
Kujikwamua kimaisha katika nyanja zote za
kimaendeleo.
B.
Kusaidiana katika hali na mali, katika
taabu na raha na kufanya matendo ya huruma kwa wanajamii wenye mahitaji
mbalimbali kama:
(i) Kuwatembelea
wafungwa magerezani wanawake na watoto;
(ii) Kuwaona
yatima na wajane katika shida zao;
(iii) Kuwafariji
wagonjwa mahospitalini;
(iv) Kutoa
ushauri kwa walioathirika na madawa ya kulevya, n.k.
C. Kuanzisha miradi ya maendeleo yenye lengo la kuhakisha kikundi kina uwezo wa kutekeleza shughuli zake;
i. Biashara ndani ya kikundi
ii. Mikopo kwa wanachama
D. Kusaidia /kushiriki katika shughuli
mbalimbali za kijamii;
E.
Upendo na Mshikamano
i.
Kushirikiana na vikundi vingine
vinavyofanya shughuli kama za kikundi hiki.
F.
Uamini na Uadilifu.
No comments:
Post a Comment